ANAYETUHUMIWA KUIBA SUKUMAWIKI ZA SH. 100 APANDISHWA MAHAKAMANI

Sukuma wiki
Sukuma wiki.
 
Na SAMUEL KARANJA
MWANAMUME mmoja amefikishwa katika mahakama moja ya Murang’a Kenya na kushtakiwa kwa kuiba sukumawiki za thamani ya Sh100.
Mshtakiwa Peter Gichuhi Gitau alikanusha kuwa aliiba mali hiyo ya Bi Elizabeth Mwangi katika kijiji cha Kiria kaunti ya Murang’a.
 
Hakimu mkuu mwandamizi Bw Joseph Masiga alimwachilia mshtakiwa kwa dhamana ya Sh50,000 au pesa taslimu Sh10,000.

Katika mahakama iyo hiyo,mwanamume mwingine alishtakiwa kwa kumnajisi msichana wa umri wa miaka 14.

Vile Vile Bw Ernest Maina Mbogo alishtakiwa kwa kumpapasa sehemu za siri msichana huyo wa shule. Hata hivyo alikanusha mashtaka hayo mawili.

Kiongozi wa mashtaka Bw Solomon Nalikha aliomba mahakama kutomwachilia mashtakiwa kwa dhamana yeyote na iwapo mahakama ingefanya hivyo, basi impe wadhamini wawili.

Hakimu alimwamchilia Bw Mbogo kwa dhamana ya Sh500, 000 na wadhamini wawili wa kiasi kama hicho. Kesi hiyo itasikizwo Agosti 20 mwaka huu.

Bastola
Katika mahakama hiyo, wanamme wengine wawili walistakiwa kwa makosa ya kumiliki bastola kinyume cha sheria.

Bw John Muru Ndegwa kwa jina jingine Paul Irungu Macharia na Cyrus Kibunja Ndung’u au John Mwangi Irungu walikanusha mashtaka hayo na kuwachiliwa kwa dhamana ya Sh500,000 kila mmoja na mdhamini wa kiasi kama hicho.

Bw Ndegwa vile vile alishtakiwa kwa kosa la kukosa kitambulisho cha taifa na kupigwa faini ya Sh15,000 au kufungwa jela miezi18 akishindwa kulipa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo