Barabara ya Koinange mjini Nyahururu
Na KNA
MWANAMUME aliyeiba Sh30,000 kutoka kwa mkewe alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu na mahakama moja mjini Nyahururu.
Patrick
Nderitu alifikishwa mbele ya hakimu mkuu, Bw Dennis Mikoyan na kukubali
kuwa alimwibia mkewe, Bi Damaris Wanjiku katika kijiji cha Gatundia,
Laikipia Magharibi nchini Kenya mnamo Mei 30, mwaka huu.
Upande wa
mashtaka uliiarifu mahakama kuwa asubuhi hiyo, mkewe mshukiwa aliacha
mkoba wake nyumbani kwao baada ya kuondoka kwenda kazini. Mwanamke huyo
huwa ni mhudumu wa benki ya Equity katika kituo cha kibiashara cha
Gatundia.
Aliporudi
kuuchukua mkoba wake, hakumkuta mumewe, ambaye alikuwa ametoroka na
mkoba huo ambao ulikuwa na pesa hizo. Aliacha ujumbe mfupi uliosema kuwa
'alikuwa ameenda kutafuta mahali pazuri pa kukaa'.
Ujumbe huo ulieleza kuwa mshukiwa angerudi baadaye na kumweleza mwanamke huyo kuwalea watoto.
Mwanamume huyo alirudi mnamo Julai 13, bila pesa hizo ambapo alikamatwa na kushtakiwa.