MWIGIZAJI
Nyota katika tasnia ya filamu Swahiliwood Jacob Stephen ‘ JB’ baada ya
kutesa katika filamu ameibuka na utambulisho wa mradi mwingine wa mavazi
JB ametengeneza fulana, top, kofia, mifuko ikiwa na nembo yake
anayoipenda ya ‘Bonge la bwana’ nguo hizo zinapatikana katika maduka
mbalimbali ya Jijini Dar es salaam na baadhi ya mikoa.
Akiongea
na FC meneja wa msanii huyo Marco Kilo amesema nembo ya msanii huyo
mkubwa katika tasnia ya filamu ni yenye ubora wa hali ya juu na wameamua
kutoa hiyo kwa ajilio ya wapenzi wa filamu ambao wanamhusudu sana JB
ikiwa kama ni sehemu ya zawadi yao kwa wapenzi wa filamu na wadau wa
filamu Bongo.
“JB ni kipenzi cha watu, kuna wakati ambao wengi upenda kupiga naye
picha wakionyesha mapenzi na msanii wao, kama uongozi tumepokea maoni
mengi wakitaka JB aweze kutoa mavazi kwa ajili ya kuitangaza nembo yake
ya Bonge la Bwana nasi kwa kuheshimu hilo tumefanya hivyo,”anasema
Killo.
Wapenzi wa filamu wataweza kujipatia tishirt, Top na vitu vingine
katika maduka mbalimbali ikiwa na alama ya JB bonge la bwana ikiwa
katika ubora wa kipekee, tumuunge mkono msanii wetu katika kujiimarisha
na kuongeza kipato.