MAAJABU:MWANAMKE ABADILIKA NGOZI NA KUWA ALBINO


Na Ibrahim Yassin,Rungwe

KATIKA  hali isiyokuwa ya kawaida iliyowashangaza wengi imetokea baada ya mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Neema Abel  Masebo (26) mkazi wa kijiji cha Igogwe kata ya Bagamoyo  wilayani Rungwe mkoani Mbeya kubadirika  ghafla kuwa mlemavu wa ngozi yaani (Albino),

Akisimulia  mkasa  huo Neema  masebo alisema kuwa alipatwa na kisa hicho siku za hivi karibuni wilayani Rungwe alipokuja kuwasalimia wazazi wake akitokea jijini  Mbeya alikokuwa anaishi,na kwamba alipo lala siku ya kwanza hasubuhi  yake aliamka akiwa amevimba mwili mzima,

Alisema kuwa  mama yake mzazi Tumaini Mlawa alipoona hali hiyo alimkimbiza katika hospital ya wilaya ya Rungwe (Makandana)kwa ajili ya matibabu ambapo alilazwa siku 7 lakini hali yake ikaanza kubadirika  kuwa mbaya huku ngozi yake ikianza kuchubuka taratibu hadi alipobadilika na kuwa  mlemavu wa ngozi yaani (Albino)

Aliendelea kusema  kuwa  baada  ya madaktari kushindwa kuzuia hari hiyo isiendelee alifika mganga wa hospitali ya serikali ya Marekani,Dr,Jescar  akiwa katika ziara ya kikazi katika hospitali hiyo alimchukua vipimo na kuvituma nchini kwake kwa uchunguzi zaidi lakini hakuletewa majibu,na badala yake alipewa mafuta ya kuzuia mionzi ya jua na kuondoa vidonda,aina ya AQUASPORT  LOTION,ambayo yamemsaidia kutokuwa na  vidonda,

Alisema  kuwa  mara  baada ya kupewa mafuta  hayo alitoka hospital huku tayari akiwa na ulemavu huo,ndipo alipotokea mama mmoja  jirani yake ambaye jina lake halikutajwa,alimpeleka kwenye kanisa la maombi la Temple of prayer for all nations church,la wilayani Kyela,na baada ya kufanyiwa maombezi ikiwa ni pamoja na kupakwa mafuta  ya upako hali yake imeanza kurejea taratibu,

Baadhi ya wakazi wa kata ya bagamoyo  wilayani Rungwe wamelihusisha tukio hilo na imani za kishirikina huku wakisema toka dunia hii ilipoanza hawajawahi kuona tukio kama hilo la mtu wa kawaida kubadilika ghafra kuwa na ulemavu wa ngozi yaani Arbino,na kuwa wanamuomba mungu ili amsaidie  na hali yake irejee kama zamani,

Mchungaji  wa kanisa hilo Nabii Charles  Mkuvasa  amekili kumpokea mgonjwa huyo kanisani kwake na kwamba  alipoletwa na mama huyo alikuwa na hali mbaya  lakini baada ya kumfanyia  maombi  na yeye kupokea  uponyaji  kutoka  kwa yesu  kristo,hali  yake sasa imeanza  kurejea taratibu  na mungu yupo pamoja naye atarejea na kuwa kama zamani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo