UVUNAJI WA SAMAKI WAONGEZEKA WILAYANI BABATI

 
Imesemekana kuwa  uvunaji wa samaki umeongezeka kwenye Wilaya ya Babati Mkoani Manyara ambapo mwaka 2005 walikuwa wanavua kiasi cha tani 102 na sasa wanavuna tani 208 za samaki.
 
Taarifa hiyo imetolewa na  Mkuu wa wilaya hiyo Khalid Mandia wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi wa CCM kwa mwaka 2005/2015  kwa waandishi wa habari na wakuu wa idara wilaya ya Babati mkoani Manyara.
 
 Alibainisha  kuwa pamoja na kufunga mabwawa hayo kwa miezi sita kisha wanayafungua pia wameanzisha na kuimarisha vikundi vya usimamizi wa rasilimali za uvuvi katika mialo.
 
 Aidha  kwa upande wa sekta ya nyuki idadi ya wafugaji nyuki  alisema kuwa imeongezeka kutoka wafugaji 1,474 mwaka 2002 hadi wafugaji 2,774 mwaka 2012 na nta kilo 2,532 zinazalishwa kwa mwaka.
 
 Aliongeza kuwa matumizi ya mizinga ya kisasa imeongezeka kutoka mizinga 199 mwaka 2005 hadi  mizinga 5,780 mwaka 2012 wakati kiasi cha asali kimeongezeka kutoka kilo 24,313 mwaka 2005 hadi kilo 67,832 kwa mwaka 2012.
 
Aliendelea kusema kuwa  sekta ya elimu imekuwa na mafanikio mwaka hadi mwaka kwani madarasa ya awali shule ya msingi yameongezeka na shule za sekondari mwaka 2005 zilikuwa 30 na hadi mwaka 2012 zilifikia shule 41.
 Alisema kuwa kwa upande wa sekta ya maji asilimia 70 ya wakazi wa mji wa Babati wanapata maji safi na salama na asilimia 60 ya wakazi walio nje ya mji wanapata maji safi na salama.
 
 Aliendela kusema kuwa   mwaka 2005 walikuwa na hospitali mbili,vituo vya afya vinne na zahanati 17 na mwaka 2012 walikuwa na hospitali tatu tatu,vituo vya afya tisa  na zahanati 39. 
 
Alimalizia kwa kusema kuwa ili kuendelea kusimamia sheria ndogo za uvuvi wenye lengo la kuongezeka kwa samaki,wilaya hiyo inaendelea kuyafunga maziwa na mabwawa waliyonayo katika kipindi cha mwezi Januari hadi Juni kila mwaka ndipo huyafungua.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo