MAGEREZA WAPATA MAFUNZO JUU YA JINSIA

 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akimsalimia  Mwezeshaji wa Mafunzo ya Jinsia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Asina Omari (kulia) kabla ya kufungua mafunzo ya Jinsia awamu ya pili mjini Morogoro leo. Kushoto ni Kamishna wa Sheria na Utawala wa Jeshi la Magereza, Dk. Juma Malewa. Pereira aliwataka maafisa wa jeshi hilo wahakikishe msongamano ndani ya magereza nchini unapungua.

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja akitoa hotuba fupi ya kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima ili afungue mafunzo ya jinsia kwa maafisa hao.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima akizungumza na maafisa mbalimbali wa jeshi la magereza kabla ya kufungua mafunzo ya jinsia kwa maafisa hao.
 Maafisa Magereza wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Pereira Ame Silima (hayupo pichani) wakati alipokuwa anatoa hotuba ya ufunguzi wa mafunzo ya jinsia mjini Morogoro.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima (wa katikati waliokaa) akiwa na Viongozi watendaji, maafisa  wa Jeshi la Magereza, wawezeshaji wa mafunzo ya Jinsia, na watumishi raia wa jeshi hilo katika picha ya pamoja baada ya ufunguzi mafunzo hayo.

PICHA ZOTE NA
 KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo