Meneja Mwendeshaji wa Kampuni ya Multchoice Tanzania, Ronald Shelukindo
(kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es
Salaam leo, kuhusu masuala mbalimbali ya kampuni hiyo. Kushoto ni Meneja
Uhusiano wa Kampuni ya hiyo Barbara Kambogi.
Na Dotto Mwaibale
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeombwa kuwachukulia hatua za
kisheria Kampuni na watu wanaorusha matangazo bila ya kuwa na hati
miliki ya kurusha matangazo hayo.
Hayo yalisema Dar es Salaam na Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multchoice Tanzania Barbara Kambogi wakati akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari.
Meneja huyo wa kampuni hiyo inayosambaza vifaa vya DSTv nchini ameiomba TCRA kuwachukulia hatua za kisheria mara moja watu hao.
Alisema kuna baadhi ya kampuni yamekuwa wakijiunganishia matangazo kutoka kwenye kampuni zinazorusha kwa kutumia satalaiti bila ya kupewa hati miliki.
"Tunaiomba TCRA ihakikishe kuwa wale wote wanaorusha matangazo
hayo wanakuwa na hati miliki ya kumruhusu kuchukua matangazo kwenye
kampuni zinazotumia satalaiti ili waweze kurusha kwenye vituo vyao" alisema Kambogi
Meneja Mwendeshaji wa Kampuni hiyo Ronald Shelukindo alisema
kwa wateja wanaotumia vifaa vya DSTv hawatakumbwa na mfumo wa kuingia kwenye digitali kwa kuwa kampuni hiyo ilishaingia kwenye mfumo huo tangu awali.
Alisema wateja wao wanatakiwa walipe kabla ya muda wa matangazo
hayo kuisha ambapo watakaokuwa wamelipia mapema watapewe asilimia 10 hivyo wata weza kuona vituo vingi vya kurushia matangazo hayo.
Hayo yalisema Dar es Salaam na Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multchoice Tanzania Barbara Kambogi wakati akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari.
Meneja huyo wa kampuni hiyo inayosambaza vifaa vya DSTv nchini ameiomba TCRA kuwachukulia hatua za kisheria mara moja watu hao.
Alisema kuna baadhi ya kampuni yamekuwa wakijiunganishia matangazo kutoka kwenye kampuni zinazorusha kwa kutumia satalaiti bila ya kupewa hati miliki.
"Tunaiomba TCRA ihakikishe kuwa wale wote wanaorusha matangazo
hayo wanakuwa na hati miliki ya kumruhusu kuchukua matangazo kwenye
kampuni zinazotumia satalaiti ili waweze kurusha kwenye vituo vyao" alisema Kambogi
Meneja Mwendeshaji wa Kampuni hiyo Ronald Shelukindo alisema
kwa wateja wanaotumia vifaa vya DSTv hawatakumbwa na mfumo wa kuingia kwenye digitali kwa kuwa kampuni hiyo ilishaingia kwenye mfumo huo tangu awali.
Alisema wateja wao wanatakiwa walipe kabla ya muda wa matangazo
hayo kuisha ambapo watakaokuwa wamelipia mapema watapewe asilimia 10 hivyo wata weza kuona vituo vingi vya kurushia matangazo hayo.