IPC YAJA YA MPANGO WA KUMILIKI REDIO YAKE

Mwenyekiti  wa  IPC Frank Leonard (kushoto) akiteta jambo la katibu mtendaji  wa IPC ,Francis Godwin
 
NA FRANCIS GODWIN
BAADA ya  kukamilisha zoezi zima la uanzishaji  wa chama cha  kuweka na kukopa  cha klabu  ya  waandishi  wa habari  mkoa  wa Iringa (IPC VIKOBA) sasa klabu  hiyo ya  wanahabari mkoa  wa Iringa imekuja na  wazo  wa  kumiliki kituo cha radio kitakachojulikana kama  Radio IPC FM. 

Mwenyekiti  mpya  wa IPC Frank  Leonard ameyasema hayo leo  wakati akifanya mahojiano  na vyombo  mbali mbali ukiwemo mtanddao  huu  wa www.francisgodwin.blogspot.com na  Zenji FM ya  Zanzibar  kuhusiana na mkakati  wa klabu  hiyo baada ya kukamilisha zoezi la uanzishwaji  wa IPC VIKOBA na  kuziba nafasi za  viongozi ndani ya klabu hiyo. 

Leonard  amesema  kuwa kutokana na nguvu inayoendelea  kuonekana ndani ya IPC kabla ya  kifo  cha aliyekuwa  mwenyekiti  wa IPC  Daud Mwangosi na sasa ni  wazi  kuwa mkakati  huo  utafanikiwa na utakuwa ni ukombozi  mkubwa kwa  wanahabari  mkoa  wa Iringa. 

Hata  hivyo  alisema  wakati akiwa  katibu mtendaji  wa IPC na Mwangosi akiwa mwenyekiti katika moja kati  ya vikao  vya kamati ya utendaji  suala  hilo la kuanzisha  kituo  cha radio  lilijadiliwa kwa  kina  japo utekelezaji  wake haukuanza ila sasa  IPC imepania  kulisimamia  wazo hilo ambalo lilitolewa chini ya  uongozi wa  Marehemu Mwangosi na kuungwa mkono na  wanachama   wote. 

Alisema  kuwa  sehemu  kubwa ya  wanachama  wa IPC ni  wanahabari ambao  wanafanya kazi  katika  vyombo mbali mbali  ila baadhi yao ni  waandishi  wa  kujitegemea hivyo iwapo IPC  itaanzisha kituo hicho cha radio  kitakuwa ni ukombozi mkubwa kwa wanahabari  wanaofanya kazi  zao kwa  kujitegemea kwa kusimamia  radio  hiyo. 

Pia  alisema  kuwa moja kati ya mipango ya kuwa na radio hiyo ni  kuweza  kutoa mfano mwema kwa  vituo  vya radio Fm hapa nchini ambazo baadhi  zinaendeshwa  kinyume na maadili ya utangazaji na  hivyo  kituo hicho cha radio IPC FM kitasaidia  kuonyesha mfano  wa namna gani radio FM  zinaweza  kuendeshwa kwa maslahi ya  jamii  zaidi badala ya   kuendeshwa kinyume na maadili. 

katika hatu  nyingine Leonard  amesema  kuwa  IPC  kwa kushirikiana na baraza la habari Tanzania  (MCT ) imeanzisha kamati ya usuluhishi  kwa ajili ya  kutoa nafasi ya  wananachi ambao  wanaripotiwa  vibaya katika  vyombo  vya habari  kuweza kufikisha malalamiko yao kwa kamati hiyo na  wahusika  kuhojiwa . 

Alisema  kamati hiyo itafanya  kazi yake kwa  wanahabari  wote bila kujali  kuwa ni mwanachama  wa IPC ama si mwanachama na  kuwataka  wananchi ambao  wataona  wameandikwa ama kuripotiwa  vibaya na chombo  chochote cha  habari  kufika  IPC ili kukutana na kamati  hiyo kabla ya kukimbilia mahakamani.

Kamati  hiyo  ya usuluhishi  inaundwa na  wajumbe nane  ikiongozwa na  wakili maarufu mkoani Iringa mheshimiwa Dismas Mmbando ambae ni  mwenyekiti  wa kamati  hiyo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo