ASKOFU ALIYEPIGWA RISASI ZANZIBAR AKANA TAARIFA YA POLISI

Padri Ambrose Mkenda wa Kanisa Katoliki Mpendae,Zanzaibar akipakizwa kwenye gari kupelekwa Uwanja wa Ndege wa Zanzibar tayari kwa kusafirishwa kwenda katika Hospitali ya Taifa Muhimbili,Dar es salaam kwa matibabu zaidi baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana Mjini Zanzibar juzi jioni. Picha Martin Kabemba.  
--
PADRI Ambrose Mkenda ambaye alipigwa risasi Jumanne iliyopita, mjini Zanzibar na watu wasiojulikana amekana maelezo yaliyotolewa na polisi yakimtaja kuwa ni Mhasibu wa Kanisa Katoliki, Zanzibar.
 
Akizungumza na waandishi wa habari katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako amelazwa, Padri huyo alisema wadhifa wake ni Mkurugenzi wa Idara ya Uchungaji anayeshughulikia masuala yote ya Kanisa Katoliki visiwani humo.

Alisema hakuwa mhasibu wa kanisa hilo kama inavyoelezwa na kwamba taarifa hizo siyo za kweli.Hata hivyo, Padri Mkenda alisema alikuwa akimsaidia mhasibu kwa kipindi cha miezi mitatu.
 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo