CUF YAHAMASISHA WANANCHI KUJIUNGA NA CHF



SIHA

Mwenyekiti wa chama cha wananchi [CUF]Wilayani Siha Mkoani Kilimanjoro amewataka viongozi wote Wilayani humo pamoja na madiwani kuhamasisha Wananchi kujiunga na mfuko wa Bima ya afya [CHF] ili waweze kupatiwa matibabu kwa uraisi zaidi

IDD Hamisi alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisi kwake jana

Alisema Wananchi sasa wanatakiwa kupewa elimu madhubuti juu ya umuhimu wa kujiunga na mfuko huo kwa kuwa unasaidia wanapopatwa na matatizo pale wanapoumwa wakati hawana fedha za matibabu

Alisema madiwani na viongozi mbalimbali wanatakiwa kua mstari wa mbele kuhamasisha Wananchi kujiunga na mfuko huo kwa kuwa ndiyo wanaoishi nao muda wote na wanafahamu vyema mazingira yao

"Nawaomba ndugu zangu madiwani na viongozi wengine tuhamasishe wananchi wetu kujiunga na mfuko wa bima ya afya ili waweze kupatiwa matibabu kiraisi na mahali popote" alisema

Alisema endapo madiwani katika harakati zao za kimaendeleo kwa wananchi wataonyesha  ushirikiano wa kuhamasisha wananchi hao kujiunga na bima hiyo basi itawezesha kujipatia matibabu yao bila shaka


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo