MAKETE           
Vijana wa wilaya ya Makete wameshauriwa kuacha tabia ya uvivu na kuchagua kazi, na badala yake kujiajiri wenyewe na kuacha tabia ya kuilaimu serikali kuwa ndiyo imesababisha ugumu wa maisha yao  

Hayo yamezungumzwa na Afisa maendeleo ya jamii Bw. Denis Sinene wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii katika ofisi ya kijiji cha Iwawa wilayani Makete

Amewataka vijana hao kuachana na tabia hiyo na badala yake wanaweza kuanzisha vikundi vitakavyowasaidia kuinua vipato vyao na kuboresha maisha yao kwani kwa kufanya hivyo itakuwa rahisi kwao kupewa mikopo

Katika hatua nyingine amewaomba wananchi kushirikiana na jeshi la polisi kutokomeza uhalifu unaofanywa na mtu binafsi au makundi hasi katika jamii
Na Obeth Ngajilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo