Kofi Annan amenza mazungumzo yake ya amani na Rais Bashar al Assad.

In this photo released by Insider Images for UN Foundation , former United Nations Secretary-General and UN Foundation Board member Kofi Annan, addresses the 'New African Connections' conference hosted in Oslo, Norway, by NORAD, CARE, and supported by the UN Foundation, Tuesday, June 21, 2011. The UN Foundation Board meeting in Norway includes discussions which focus on ways to help new partners connect with the lifesaving work of the United Nations. (AP Photo / Stuart Ramson/Insider Images for UN Foundation, HO) NO SALES NORWAY OUT
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Waarabu Kofi Annan amenza mazungumzo yake ya amani na Rais Bashar al Assad.

Annan ambae amekwisha wasili nchini humo muda mfupi uliopita, pia anatarajiwa kukutana na upande wa upinzani kabla ya kuondoka hapo kesho. Awali hapo jana vikosi vya Syria vimeuwa kiasi ya watu 68 baada ya maelfu ya watu kuingia mitaani katika maeneo tofauti katika maandamano yaliyofanyika katika maeneo tofauti.

Mauwaji hayo yanafanyika siku moja tu, kabla kuwasili kwa Annan. China imetuma ujumbe wake mpya katika nchi za Kiarabu na Ufaransa katika juhudi zake za kutaka kusitishwa mapigano nchini Syria.

Pamoja na hayo China bado inapinga pendekezo la mataifa ya kigeni kuwatuma wanajeshi Syria.

Baada ya kuwatembelea wakimbizi wa Syria nchini Uturuki, Mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa Valerie Amos alisema serikali ya Assad imekubali kujiunga na mashirika ya Umoja wa Mataifa kufanya tathmini ya kiasi fulani kwa mahitaji ya raia nchini Syria, lakini haikukubali kuhusu suala la kuyaruhusu makundi ya misaada kuingia maeneo ya machafuko bila ya ruhusa. 

Na DW        


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo