KWA NINI WASANII WAKONGWE WANAZIKATAA TUZO ZA KILI?

 
 
Mara baada tu ya kutangazwa kuwa mmoja wa watakaoshiriki kupigiwa kura kwenye hatua ya awali ya mchujo wa tuzo za BASATA KILIMANJARO MUSIC AWARDS, msanii  wa bongo fleva Dully Sykes amekuja juu na kulaumu wahusika kwa kitendo chao cha kumuweka katika kinyang'anyiro hicho wakati alishasema hataki siku nyingiiii.
 
"Nilishawaambia sitaki kuwepo tena katika tuzo zao, tangu mwaka juzi, lakini nashangaa kuona wanaendelea kuniweka tu, kwani wananiona mimi ndio msanii pekee, wakati ule wa hits kama nyambizi, Hi na zinginezo mbona hawakunipa tuzo? au walidhani mi ni msanii ambae ningeishia kati tu, lakini baada ya kuona nipo na naendelea kuwepo ndio wanajifanya kunitambua..nimesema sitaki.
 
Hata hivyo baada ya BASATA kuulizwa kuhusu tuhuma hizo walisema msanii kama hataki kuwemo kwenye tuzo hizo basi aandike barua BASATA ya kujitoa lakini sio kwa maneno tu.
 
SOURCE: PRO 24 DJS


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo