Makete                     08.02.2011

Wadau mbalimbali wa utekelezaji wa mradi wa Tmf ambao ni Wafanyakazi wa Kitulo Fm, PIUMA na MASUPHA wamejengewa uwezo wa namna ya kuandaa vipindi vya redio na namna ya kutekeleza mradi huo

Lengo la mradi huo ni kuongeza uelewa kwa jamii ya Makete juu ya Uchangiaji wa mila na desturi katika maambukizi ya VVU, matunzo na huduma kwa watoto yatima na wenye VVU kupitia vipindi vya redio

Akizungumza na washiriki hao mkufunzi wa mafunzo hayo Bw. Charles Kayoka amesema kuwa malengo ya mradi huo ni vyema yakatekelezwa kwa ufanisi unaotakiwa ili kuisaidia jamii ya wanamakete na wote watakaokuwa wakisikiliza vipindi hivyo

Aidha amewataka watangazaji hao kuandaa vipindi vilivyobora na vyenye kuigusa jamii kwa kuwashirikisha wanajamii wenyewe na wadau mbailmbali watakaohitajika

Kwa upande wao washiriki hao wamesema wako tayari kuutekeleza mradi huo ipasavyo na kuomba wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha kwao pindi watakapoanza kupita maeneo mbalimbali ya wilaya ya Makete ili kutekeleza mradi huo ikiwemo kuandaa vipindi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo