USHIRIKIANO BAINA YA WAZAZI NA WAALIMU UNAHITAJIKA KUINUA ELIMU MAKETE

Wananchi wilayani Makete wametakiwa kutoa ushirikiano dhidi ya changamoto zinazowakabili waalimu pindi wanapotakiwa kufanya hivyo kwani kwa kufanya hivyo kutaleta ufanisi katika jamii

Hayo yamezungumzwa na baadhi ya maafisa ustawi wa jamii wilaya ya Makete walipofanya ziara katika shule ya msingi Makete na kubaini changamoto mbalimbali zilizopo shuleni hapo ikiwa ni pamoja na kukosekana ushirikiano baina ya wazazi na waalimu, uchache wa waalimu, pamoja na uhaba wa vitendea kazi ikiwemo vitabu na chaki

Changamoto nyingine zilizobainika ni pamoja na baadhi ya wawazi na walezi kukataa kuitikia wito pindi wanapoitwa shuleni kwa ajili ya vikao ama mazungumzo yanayohusu maendeleo ya watoto wao

Miongoni mwa Maafisa Ustawi hao aliyejitambulisha kwa jina la Denis Sinene amewaasa wanafunzi hao kuacha vitendo viovu ikiwa ni pamoja na kuacha utoro, na kuwataka kusoma kwa bidii

Na Aldo Sanga & Riziki Manfred


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo