Young Africans yashtakiwa TPLB

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasilino ya Bodi ya Ligi ‘TPLB’ Karim Boimanda amekiri kupokelewa kwa malalamiko kutoka kwa Wadau wakiilalamikia klabu ya Young Africans kuvunja kanuni kwa kuvaa Jezi nyeusi mfululizo.


Young Africans imefululizo kuvaa Jezi za rangi nyeusi kwa Michezo ya nyumbani na ugenini ya Ligi Kuu, halia mbayo imeleta tahariki hadi malalaiko hayo kufikishwa Bodi ya Ligi ‘TPLB’.


Boimanda amesema jambo hilo litafanyiwa kazi na kama Young Africans watakuwa wamevunja kanuni, na adhabu yake ni faini Shilingi milioni moja.


Ameongeza klabu zinatakiwa zivae Jezi kulingana na jinsi walivyozitambulisha, Nyumbani, Ugenini na Jezi ya Tatu ambayo unaruhusiwa kuvaliwa sehemu yoyote ikiwa imetokea mgongano wa rangi za Jezi na pinzani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo