Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma limeazimia kumuita mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kanali Laban Thomas kwenye kikao cha dharula ili wamueleze kero nne zinazoisumbua jamii ikiwemo ya wafugaji ambao inadaiwa kuna baadhi ya watumishi wasio waaminifu kugeuza mitaji kutoka kwa wafugaji.
Wakichangia kamati ya huduma za uchumi kwenye Baraza hilo walisema kuwa swala la mifugo wilayani humo limekuwa kero kubwa sana licha ya Mkurugenzi kuunda kikosi kazi kwaajiri ya kufanya operesheni ya kuwafukuza wafugaji hao lakini bado hali imekuwa mbaya na idadi ya mifugo inazidi kuongezeka Jambo ambalo linaleta kero kwa wakulima na kutishia uwepo wa njaa.
Walisema kuwa wakulima walayani humo wamekosa msaada licha ya kutoa malalamiko yao serikalini juu ya uhalibifu unaofanywa na wafugaji lakini pia kunawanyama waalibifu kama Tembo nao huvamia mashamba na kufanya uharibifu mkubwa hivyo wameamua kikao hicho kigeuke kamati na maazimio waliyoyatoa wanamuhitaji mkuu wa Mkoa ili akawasikilize kero zao.
Kwa upande mwingine wameitaka Serikali kuiondoa Wilaya ya Tunduru kwenye mfumo wa kuuza zao la mbaazi kwa kutumia mfumo wa Stakabadhi ya mazao ghalani kama ilivyo fanyika katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kwani hakuna faida wanayopata.
Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma limeazimia kumuita mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kanali Laban Thomas kwenye kikao cha dharula ili wamueleze kero nne zinazoisumbua jamii ikiwemo ya wafugaji ambao inadaiwa kuna baadhi ya watumishi wasio waaminifu kugeuza mitaji kutoka kwa wafugaji.
Wakichangia kamati ya huduma za uchumi kwenye Baraza hilo walisema kuwa swala la mifugo wilayani humo limekuwa kero kubwa sana licha ya Mkurugenzi kuunda kikosi kazi kwaajiri ya kufanya operesheni ya kuwafukuza wafugaji hao lakini bado hali imekuwa mbaya na idadi ya mifugo inazidi kuongezeka Jambo ambalo linaleta kero kwa wakulima na kutishia uwepo wa njaa.
Walisema kuwa wakulima walayani humo wamekosa msaada licha ya kutoa malalamiko yao serikalini juu ya uhalibifu unaofanywa na wafugaji lakini pia kunawanyama waalibifu kama Tembo nao huvamia mashamba na kufanya uharibifu mkubwa hivyo wameamua kikao hicho kigeuke kamati na maazimio waliyoyatoa wanamuhitaji mkuu wa Mkoa ili akawasikilize kero zao.
Kwa upande mwingine wameitaka Serikali kuiondoa Wilaya ya Tunduru kwenye mfumo wa kuuza zao la mbaazi kwa kutumia mfumo wa Stakabadhi ya mazao ghalani kama ilivyo fanyika katika kipindi cha miaka miwili iliyopita kwani hakuna faida wanayopata.
