Breaking News: Mtangazaji mwingine wa EFM afariki Dunia

Taarifa zilizotufikia hivi sasa ni kwamba Mtangazaji wa EFM Denis Rupia maarufu kama Chogo amefariki dunia

Taarifa hizi zimetolewa na Meneja Mkuu wa EFM Denis Sebo jukwaani usiku huu wakati wa Tamasha la Muziki Mnene linalofanyika Mubashara jijini DSM

Hali hiyo imepelekea matangazo hayo ya moja kwa moja kukatishwa

Hii hapa chini ndiyo taarifa ya awali iliyotolewa na EFM

"Uongozi na Wafanyakazi wa E-FM,TV-E kwa majonzi na masikitiko makubwa tunatangaza kuondokewa na Mwanafamilia Mwenzetu Dennis Rupia (Chogo),aliyefarika Dunia baada ya kuugua kwa kipindi cha muda mfupi.

Aidha kwa taarifa zaidi tataendelea kufahamishana taratibu za kumpumzisha mpendwa wetu kupitia vyanzo mbalimbali vya mawasiliano.

Hakika ni kipindi Kigumu kwetu,Wasikilizaji wa Redio na familia kwa ujumla tuendelee kuombea Mpendwa wetu" ,E-FM.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI-AMEN


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo