Mwenyekiti wa Kijiji afariki baada ya kusikia mchungaji wake kafa kwa Ajali

Image may contain: one or more people and outdoorNa Maiko Luoga Ludewa
mwenyekiti wa kijiji cha Mkiu katika kata ya Lubonde wilayani Ludewa kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Bw.Kretus mtewele Amefariki Dunia Usiku wa kuamkia Leo January 25 katika hospital ya misheni Lugarawa.
Taarifa kutoka kwa diwani wa kata hiyo Mh. Nicholaus Mgaya (CCM) zinasema kuwa Marehemu Alipatwa na mshtuko mkali baada ya kupokea Taarifa za Kifo cha mchungaji Frenk Ngatunga wa kanisa Anglican mtaa wa kiyombo aliyefariki kwaajali ya Pikipiki iliyotokea January 22 mchana mwaka huu huko katika kijiji cha mkiu Barabara ya kuelekea Kiyombo.
Mh Mgaya amesema kuwa Anafanya kikao kidogo cha mazungumzo na watumishi wa kata yake asubuhi hii ili kuweza kukamilisha taratibu za kusafirisha mwili wa marehemu pamoja na Taratibu za Mazishi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo