AUDIO: Ambulance Yazua Gumzo Baraza la Madiwani Makete

Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Makete limeagiza kurudishwa haraka dereva wa gari la kubebea wagonjwa maarufu kama ambulance la kituo cha afya Ipelele

Baraza hilo limeagiza hadi kufikia  Januari 27 dereva huyo aliyeondolewa katika kitu chake cha kazi kufuatia upungufu wa madereva katika halmashauri anaripoti kituoni hapo na aendelee na kazi

Maagizo hayo yanafuatia maagizo ya baraza liilopita kupewa taarifa kuwa  gari hilo halifanyi kazi na mrejesho uliotolewa katika baraza hilo unaonekana kutomridhhisha diwani wa kata hiyo Mh Mwipelele Mbogela

Hali hiyo ikapelekea baraza hilo kutoka na maamuzi ya kutaka dereva arudishwe kituoni hapo na wananachi waendelee kupata huduma za afya hasa kutokana na umuhimu wa gari la wagonjwa kama alivyoeleza Mwenyekiti wa Halmashauri Mh Egnatio Mtawa

Sikiliza Sauti Hizi hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo