Waziri Nchemba aamuru wafungwa wahamishwe Gereza


Image result for gereza jirani la MwisaNa Editha Karlo wa blog ya jamii,Kagera.


WAZIRI 
wa mambo ya ndani ya nchi Mwigulu Nchemba amemtaka mkuu wa magereza 
mkoa wa Kagera(RPO) kamishna mwandamizi Jeremiah Nkonda kuwahamisha 
wafungwa walioko katika gereza la Kitengule la wilayani Karagwe na 
kuwapeleka gereza jirani la Mwisa,Kutokana na tetemeko la ardhi 
lililo tokea hivi karibuni mkoani hapa na kuharibu miundombinu na 
mabweni ya kulala wafungwa katika gereza hilo.

Waziri Nchemba 
alisema kauli hiyo baada ya kufanya ziara ya siku moja  Mkoani hapa 
na kutembelea taasisi zilizo chini ya wizara yake Kwa lengo la kuona 
uharibifu uliojitokeza kutokana na tetemeko hilo . 

"Nimetembelea 
magereza yetu lakini gereza la Kitengule limeharibika sana, kuta 
zimeanguka mabweni yameharibika  Kwa kiwango kikubwa kiasi kwamba 
hawapaswi kuishi watu kwa hiyo,naagiza mkuu wa magereza hapa kuwahamishia
wafungwa hawa katika gereza la Mwisa lenye mabweni manne yaliyoko  
wazi"Alisema Nchemba.

Alisema ndani ya wiki moja zoezi hilo liwe 
limekamilika kwani wakiendelea kuwaaacha wafungwa hao humo ni hatari 
kwani wanaweza kudondokewa na kuta zinazoning'inia na kusababisha 
kuwapoteza watu hao.

Alisema kutokana na tukio hilo Wizara 
inaandaa mpango wa Muda mrefu wa kujenga bweni kubwa litakalokuwa na 
uwezo wa kubeba wafungwa 400 Kwa wakati mmoja kwani hilo ni gereza  la 
kikazi ambalo linabeba watu wengi. 

Mkuu wa magereza mkoa wa 
Kagera kamishna mwandamizi Jeremiah Nkonda alisema kilichochangia Sana 
kushuka Kwa kuta hizo ni kwamba matofali yaliyojenga kuta hizo 
yanaonekana yalijengwa Kwa tofali mbichi kwahiyo Kwa halii hiyo 
haitowezekana kufanya ukarabati bali nikuhakikisha Wamebomoa mabweni 
hayo na kujenga upya.

Alisema gereza hilo lilikuwa na uwezo wa 
kubeba wafungwa 380  Kati ya hao 100 wako Kwenye kambi ndogo ambapo 280 
ndo watakaohamishiwa katika gereza la Mwisa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo