Diwani wa CHADEMA Makete atekeleza kwa vitendo "HAPA KAZI TU"

Shule ya msingi Mafiga iliyopo katika kijiji cha Missiwa kata ya Ipelele tarafa ya Magoma wilayani Makete imepokea msaada wa madawati 10 kutoka kwa diwani wa kata hiyo kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA) yenye thamani ya sh.laki nne na nusu(450,000/=)

Akikakabidhi msaada huo jana diwani wa kata ya Ipelele Mh.Mwipelele Mbogella amesema msaada huo ni sehemu ya kuwashukuru wapiga kura wake kutokana na kuwa ni kijiji cha kwanza kilichompa kura nyingi katika uchaguzi mkuu wa mwaka uliopita.


Mh.Mwipelele pia amesema ataendelea kuwashirikisha wadau na wananchi kwa ujumla katika masuala mbalimbali ya kijamii kwani anaamini kuwa wapo tayari kumuunga mkono.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo wa madawati mkuu wa shule ya msingi Mafiga Bw.Efrahimu Sinene amemshukuru diwani huyo kwa msaada huo na kuomba azisaidie na shule zingine ili ziweze kuondokana na changamoto ya upungufu wa madawati.

Kwa upande wake afisa mtendaji wa kata ya Ipelele Bi.Anna Sanga amesema kuwa kata hiyo ina upungufu wa madawati 140 na kusema kuwa wakati wa kukabidhi msaada huo wa madawati Mh.Mwipelele alisema ni maalum kwa ajili ya kuwashukuru wapiga kura wake na ameamua kutoa msaada huo kwenye taasisi ili iweze kunufaika jamii nzima badala ya mtu mmoja mmoja.


Aidha Bi.Anna Sanga ametoa shukrani kwa diwani huyo kwa jitihada zake anazoendelea kuzifanya na kuahidi kuwa yupo tayari kushirikiana naye kwa kushirikisha wadau mbalimbali ili kuzitatua changamoto hizo.
Na Fadhili Lunati


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo