Tume ya Taifa ya uchaguzi imekutana na Kamati Maalumu inayoundwa na wajumbe kutoka vyama nane vilivyo na wagombea wa urais na makamu kuandaa Ratiba ya mikutano ya hadhara kurahisisha kubaini vyama vilivyopanga mkutano mmoja katika mkoa mmoja, wilaya moja, na Eneo moja kwa Tarehe moja.
Mkurugenzi wa NEC Kailima Ramadhani amesema anafarijika sana na ushirikiano wanaouonesha Wawakilishi Wa vyama katika kuhakikisha mchakato kuwa wa Amani na utulivu bila kujali itikadi za vyama vyao kikao kimeendelea kutwa nzima ya leo hadi kufikia makubaliano ya Ratiba kwa vyama vyote.