Magazeti ya leo July 15 2015 yana headlines pia kuhusu stori ya UKAWA kuamua kwamba watamtangaza Mgombea wao ndani ya wiki moja kuanzia sasa.. Ukurasa wa @Twitter wa Gazeti la MWANANCHI wameandika pia mwendelezo wa hiyo stori kuhusu ishu ya Viongozi wa CUF kutoshiriki kwenye Mkutano wa UKAWA jana.
Tweet1 >>>> “Mkutano wa #CUF na waandishi umeanza hivi sasa katika Makao Makuu ya #CUF kuelezea kinachoendelea ndani ya #Ukawa”
Tweet2 >>>> “#Sakaya: CUF hatukuweza kushiriki katika kikao cha jana kutokana na sababu za kikatiba ndani ya chama #MaamuziUkawa, #MkutanoCUF”
Tweet3 >>>> “#Sakaya: Maamuzi magumu ya chama huamuliwa na vikao vya maamuzi ndani ya chama, tunaendelea na vikao vya ndani ili kuwa na maamuzi ya pamoja”
Tweet4 >>>> “#Sakaya: Hatujasusia au kujitoa #Ukawa, hizo taarifa ni za uzushi na uongo, tumeona tuweke mambo ya chama vizuri ili tuende tukiwa wamoja”
