WAANDISHI wa habari wa mjini Dodoma, wamenusurika kushambuliwa kwa
kipigo na Mwenyekiti wa Kijiji cha Kongogo, Daud Husein baada ya
waandishi hao kubaini maonevu na ubabe anaowatendea wananchi.
Mwenyekiti huyo, aliwashabulia waandishi kwa matusi na maneno makali
huku akiwabeza kuwa ni makanjanja kwa madai kuwa wasingeandika kero za
wananchi bali matendo yake.
Alisema kuwa waandishi hao walitakiwa kuwapuuza walalamikaji kwa madai
kuwa aliwakarimu waandishi, hivyo hawakuwa na sababu ya kuandika uozo
wake. Hali hiyo ilijitokeza kabla kuanza kwa mkutano wa kijiji cha
Kongogo na vijiji vya jirani ambao lenga lake lilikuwa ni kupinga mradi
wa ujenzi wa lambo la kunyweshea mifugo ambalo wananchi wanalipinga
wakidai hawajashirikishwa.
Kwa pamoja wananchi wa vijiji vya Tinahi, Asanje, Babayu na Kongogo
walisema mtendaji wa kijiji cha Kongogo amekuwa akiwaburuza na
kujiamria mambo yake.