RIYAMA AKERWA NA TABIA YA WASANII WENZAKE KULETA MAIGIZO KWENYE MSIBA, ADAI AKIFA ASISIFIWE

RIYAMA Ali mwigizaji wa kike asiye na kashifa katika tasnia ya filamu Bongo, amefunguka kwa kusema kuwa kama kuna msanii mwenzake au mtu mwenye mapenzi naye angependa kama ana sifa kuhusu yeye katika umahiri wa kuigiza na mengineyo basi atumie nafasi hiyo akiwa hai, haitaji kusifiwa akifariki kwani anaamini kuwa sifa hizo hatasikia.

 “Nasema mapema kabisa sitaki kusifiwa nikifa, sifa mtu uipate ukiwa hai kama ni faida au kufurahia mwenyewe ujionee lakini nimeshafumba macho kuna faida gani, sisikii sioni haya ya nini kwangu miye?,”anasema Riyama.

Msanii huyo amesema kuwa imekuwa tabia kwa baadhi ya wasanii kuleta maigizo katika misiba ya wasanii inapotokea mara nyingi waonapo televisheni ujipanga kwa ajili ya kuhojiwa na waandishi basi hata kama marehemu alikuwa na ugomvi naye basi atajifanya jana kabla ya umauti walikuwa wote na kumwachia usia kama rafiki.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo