MSICHANA ALIYEPEWA MATESO MAKALI NA KUCHOMWA NA PASI ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI

Msichana  Yusta Lucas wa miaka ishirini aliyefungiwa ndani kwa miaka mitatu huku  akipewa adhabu ya kung'atwa na kuchomwa na pasi ameruhusiwa kutoka hopitalini baada ya hali yake kuendelea vizuri huku jeshi la polisi likikamilisha uchunguzi na mtuhumiwa kufikishwa mahakamani tarehe 11 Juni mwaka huu.

ITV imefika katika hospitali ya Mwananyamala alikokuwa amelizwa Yusta Lucus na kukutana na ndugu zake akiwemo mama ake mzazi ambaye amefafanua kwa uchungu hali aliyomkuta nayo binti yake na hatua alizochukua mara baada ya kupokea taarifa za tukio hilo.

Kaka wa Yusta licha ya kutoa shukrani kwa msamaria aliyetoo habari za mdogo wake kwa jeshi la polisi ameelezea kuendelea kusikitishwa na kitendo hicho cha kinyama na kutoa wito kwa Watanzania kuwa na moyo wa kusaidia wale wote wanaopatwa na matatizo kama hayo.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni Camillius Wambura amesema tayari uchunguzi umeshakamilika ikiwemo kumpima akili mtuhumiwa na tayari shauri hilo liko kwa mwanasheria mkuu wa serikjali na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani tare 11 Juni mwaka huu.
 
 CREDITS:ITV


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo