BRAZIL YAPONEA CHUPUCHUPU KUAGA MASHINDANO YA KOMBE LA DUNIA USIKU HUU

Brazil imeponea kung'olewa kutoka mashindano ya kombe la dunia yanayoendelea nchini humo.


Hii ni baada ya mechi ya kwanza ya mkondo wa muondoano kati yake na Chile kumalizika kwa mikwaju ya Penalti baada ya timu hizo mbili kwenda sare ya bao moja baada ya kipindi kizima cha mechi.

Na pia baada ya kucheza muda wa ziada.


Wakati wa mikwaju ya Penalti, Brazil iliingiza tatu huku Chile ikiingiza mbili.


Wakati wa mechi , Brazil iliingiza bao la kwanza la mechi ndani ya kipindi cha kwanza, lakini Chile ilileta jibu kabla ya kipindi cha kwanza cha mechi kukamilika.


Brazil ilikuwa na kibarua kigumu na shinikizo tele kutoka kwa mashabiki wa Brazil ambao walijaa uwanjani na pia kwa kuwa Brazil ni mwenyeji wa michuano hiyo ,matarajio ya wengi nchini Brazil ni kuwa wanatafanya vyema katika mashindano hayo.


Crucial moment: Gonzalo Jara (left) watches on as his penalty strikes the post and eliminates Chile
Mchezaji wa Chile akipiga penalti ambayo iligonga mwamba na kurudi uwanjani na kuipa tiketi Brazili kutinga robo fainali ya kombe la dunia nchini Brazili baada ya kazi nzuri waliyoifanya dakiak 120 na kutoka sare ya 1-1.

Distraught: Heartbroken Chile applaud their devastated fans inside the Estadio Mineirao after losing to Brazil
Kufungwa kubaya,wachezaji wa Chile wakitoka uwanjani kichwa chini baada ya kutolewa kwa penalti na Brazili katika michuano ya kombe la dunia inayoendelea huko nchini Brazili.

Safe hands: Julio Cesar saved two penalties for Brazil to help them reach the World Cup quarter-finals
Shujaa wa Brazili mlinda mlango Julio Cesar aliokoa mikwaju miwili ya penalti dhidi ya Chile na kuisaidia timu yao kutinga hatua ya robo fainali.

Hero: Cesar (centre) was hoisted high by Brazil's players in amongst the wild celebrations in Belo Horizonte Wachezaji wa Brazili wakimpongeza mlinda mlango wao Julio cezar baada ya kuokoa mkwaju wa kwanza wa penalti kutoka kwa Chile.
Tears of joy: David Luiz is tearful after his opening goal for Brazil in their last 16 clash against Chile  Beki wa Brazili David Luiz akishangilia goli lake la penalti dhidi ya Chile.
BRAZIL 
Umoja ni nguvu,baada ya dakika 120 sasa wabrazili wanakumbatiana kutiana moyo kuelekea kwenye mikwaju ya Penalti.
 Heart-stopping moment: Brazil's poster boy Neymar (centre) receives treatment as he struggles with fatigue  Baada ya dakika 90 za maumivu sasa vijana wanajipanga kwa dakika 120 ili kutafuta mshindi wa kutinga hatua ya robo fainali ya kombe la dunia 2014.
 Strapped up: Gary Medel receives treatment for a muscle injury during half-time of extra-time on Saturday  Mpambano ulikua siio mchezo ndani ya dakika 120, huyo hapo juu ni msukuma ndinga wa Chile akigangwa baada ya kupata mshike mshike uwanjani.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo