WAGOSI WA KAYA WATANGAZA KURUDI TENA KWENYE GEMU MWAKA HUU

Kundi la Wagosi wa Kaya kutoka Tanga ambalo liliwavuta mashabiki wengi Tanzania kwa nyimbo zenye ujumbe wa maisha halisi ya Kitanzania mwaka 2001 walipotoa album ya Ukweli Mtupu, limepanga kurudi tena mwaka huu.

Kundi hilo linaloundwa na Mkoloni na Dr. John, limeanzisha ukurasa mpya wa Facebook ikiwa ni sehemu ya miradi ya ujio wao ili waweze kuwa karibu zaidi na mashabiki wa sasa ambao wengi wako kwenye mitandao ya kijamii.
“BAADA YA KUTOREKODI KWA PAMOJA KAMA KUNDI KWA MIAKA 8,SASA WAGOSI WA KAYA TAYARI TUMESHAREKODI NYIMBO KADHAA AMBAPO WIKI HII TUNATARAJIA KUTAMBULISHA KAZI TULIZOFANYA UKIZINGATIA UKIMYA WA MUDA MREFU ULIOKUWA UMETAWALA KATIKA MUZIKI WETU WA HIP HOP........stay tuned!” Wagosi wa Kaya wameandika kwenye ukurasa wao wa Facebook uliopokelewa na comments nyingi za mashabiki wanaotamani kusikia tena kutoka kwao.
 
Huenda ‘Gahawa’ likawa ni jina la wimbo wao mpya kwa kuwa ndio jina liliwekwa mbele kwenye picha yao ya pamoja.
Post nyingine za Wagosi wa Kaya zinaonesha kuwa audio za nyimbo zao zitaambatana na video.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo