Kwa
hivi sasa bila kuficha wala kuupindisha ukweli, serikali haikwepi
pongezi kwa kuboresha barabara kutoka Njombe - Makete kwa kuwa awali
hali ilikuwa mbaya
Kiufupi
tangu niingie kwenye wilaya hii mwaka 2008 hali ya barabara ilikuwa
mbaya kiasi kwamba kutoka Makete hadi Njombe ilikuwa zaidi ya masaa 12
hasa wakati wa masika
Kwa
kawaida kutoka Makete hadi Njombe ni umbali wa kilomita 110, ukisafiri
kwa basi ni takriban masaa 3 hadi 5 unakuwa umefika, kwa kipindi hicho
ilikuwa ndoto kusafiri kwa masaa hayo tofauti na sasa unakwenda Njombe
na kurudi
Miongoni
mwa maeneo yaliyokuwa korofi kwa kipindi hicho cha mwaka 2008 ni Mago,
Tandala, Usungilo na Mang'oto ambapo ilikuwa ni jambo la kawaida kwa
abiria kushuka na kusukuma magari wanayosafiria na pia magari lazima
yawe na chepe na kamba kwa ajili ya shughuli hiyo
Tujukumbushe tulipotoka kupitia picha hizi ambazo zilipigwa mwezi machi 2008 kwa kweli hali ilikuwa mbaya:-
Jionee mwenyewe hali ilivyokuwa.
Abiria wakishirikiana kwa pamoja kulivuta basi lao lilipokwama meneo ya Usungilo
Kwa
sasa eneo hili lililopigwa picha hizi limewekewa lami na hakuna
usumbufu huu tena katika eneo hilo na barabara ya Njombe makete kwa
ujumla inapitika misimu yote ya mwaka bila usumbufu kama ilivyokuwa
kipindi cha nyuma
Ama
kweli jitihada za mbunge wa jimbo la Makete Dkt. Binilith Mahenge na
wadau wengine walilivalia njuga suala hili hadi barabara hii ikawekewa
lami katika maeneo yale korofi kama unavyoona hapo juu na kusababisha
usafiri kuwa mrahisi kuliko ilivyokuwa kipindi cha nyuma
Imeandaliwa na Edwin Moshi.


