Shirikisho la soka nchini TFF limetangaza kusogeza mbele
hatua ya kwanza ya usajili wa wachezaji kwa msimu wa mwaka 2013/2014
hadi August 05 badala ya August 03 kama ilivyokuwa ikionyesha katika
kalenda ya matukio.
Katibu mkuu wa TFF Angetille Osiha amesema uamuzi wa kusogeza mbele umetokana na kuchelewa kwa santuri ya usajili wa msimu huu ambayo ndiyo inayotumika kwa usajili wa elektroniki unaofanywa kwa wachezaji wa klabu za ligi kuu ya soka Tanzania bara.
Angetille Osiah amesema santuri hiyo ambayo hutolewa na kampuni ya NAS Technology ya Tunisia tayari imeshawasili nchini mpaka majira ya mchana hii leo walikuwa wakiifanyia kazi.
Katibu mkuu wa TFF Angetille Osiha amesema uamuzi wa kusogeza mbele umetokana na kuchelewa kwa santuri ya usajili wa msimu huu ambayo ndiyo inayotumika kwa usajili wa elektroniki unaofanywa kwa wachezaji wa klabu za ligi kuu ya soka Tanzania bara.
Angetille Osiah amesema santuri hiyo ambayo hutolewa na kampuni ya NAS Technology ya Tunisia tayari imeshawasili nchini mpaka majira ya mchana hii leo walikuwa wakiifanyia kazi.