YANGA KUIVAA URA KESHO

Timu ya Young Africans kesho itashuka katika dimba la uwanja wa Taifa kucheza na timu ya URA kutoka nchini Uganda ikiwa ni mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaotumiwa na watoto wa jangwani kuwatambulisha wachezaji wake wapya wa msimu huu.

Young Africans ambayo ina wiki mbili sasa tangu ianze mazoezi ya kujiandaa na msimu mpya, imeshacheza michezo mitatu ya kirafiki kanda ya ziwa miwili ikiwa ya kimataifa na mchezo mmoja ikicheza na timu iliyopanda daraja msimu Rhino Rangers ya mjini Tabora.

Mara baada ya mazoezi ya leo Kocha mkuu Ernie Brandts amesema anashukuru kikosi chake kipo fit, hakuna majeruhi na wachezaji wote wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo wa kesho ambao watautumia kama sehemu ya maandalizi ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu 2013/2014.

Brandts anatarajia kuwatumia wachezaji wake wote wa zamani na wapya waliosajiliwa kwa ajili ya msimu huu ambao ni:

1. Deogratius Munishi 'Dida' - Mlinda mlango kutoka Azam
2. Rajab Zahir - mlinzi wa kati kutoka  Mtibwa Sugar
3. Hamis Thabit - kiungo kutoka Ureno
4. Shaban Kondo - mshambuliaji kutoka Msumbiji
5. Brendan Ogbu - mshambuliaji kutoka Hertland ya Nigeria ambaye yupo kwenye majaribio


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo