skip to main |
skip to sidebar
UMASIKINI WACHANGIA ONGEZEKO LA UTAPIAMLO NCHINI
Kudorora
kwa uchumi na kukosa elimu sahihi ya lishe bora kwa jamii kumechangia
kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa idadi ya wagonjwa wa utapiamlo kwa
jamii.
Idadi ya watoto wanaopoteza maisha kutoka na ugonjwa huu imefikia watoto 130 kila siku kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2012.
Idadi hii ambayo inahofiwa kuongezeka kila kukicha inakuja huku
Tanzania hapo kesho itaungana na nchi zingine duniani katika kuadhimisha
siku ya utapiamlo Duniani.
Kasi ya
kukua kwa kiwango cha umasikini miongoni mwa watanzania kumeendelea
kuwa chanzo kikubwa cha ongezeko la ugonjwa wa utapiamlo nchini.
Asilimia 42 ya watoto wa Tanzania chini ya umri wa miaka 18 wana utapiamlo huku idadi hii ikihofiwa kuongezeka.
Kwa mujibu wa daktari wa wodi ya watoto wanaougua utapiamlo katika
hospitali ya rufaa bugando jijini Mwanza dakta Julieth Kibirigi,tatizo
la ugonjwa huo linachangiwa na kutozingatia mlo kamili kwa watoto.
Katika wodi hii watoto watano hadi saba hupokelewa kila siku wakiwa na tatizo la ugonjwa huu.
Jitahada zinazofanyika hapa nikuhakikisha watoto wanapata tiba
kamili ya ugonjwa huu lakini pamoja na jitihada hizi bado kuna
changamoto kadha wa kadha.
Katika kipindi cha miaka 5 zaidi ya watoto laki mbili na elfu thelathini na nne walipoteza maisha kutoka na ugonjwa huu nchini
Tanzania, sababu zingine ambazo ni chanzo la ongezeko la ugonjwa ni
pamoja na Bajeti ya afya kidogo ya serikali, upungufu wa vitamini na
madini kwa kina mama wajawzito,huduma duni ya afya kwa watoto wachanga.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi