Jengo hilo lilikuwa na ghorofa zaidi ya zilizoruhusiwa
Maafisa wa polisi hapa nchini wanasema kuwa takriban maiti
thelathini wamepatikana kutoka kwa vifusi vya jengo lililoporomoka jijini
Dar es Salaam Ijumaa.
Hadi sasa watu kumi na saba pekee ndio wamepatikana wakiwa hai katima jengo hilo.
Watoto waliokuwa katika uwanja wa kuchezea uliopakana na jengo hilo, walikuwa miongoni mwa waathiriwa.
Polisi wanasema kuwa wamewakamata watu wanne
baada ya rais Jakaya Kikwete kutembelea eneo la janga na kuwataka
maafisa wa utawala kuwachukulia hatua waliohusika na ujenzi huo.