| Mtoto aliyenusurika kifo |
| Mfereji unaotiririsha maji na kusababisha nyumba hiyo kubomoka |
| Mwenye nyumba hiyo akionyesha mfereji unaomwaga maji juu ya nyumba yake |
| Wananchi pamoja na viongozi wa mtaa Mabida Mlandege mjini Iringa leo |
Tukio hilo limetokea majira ya saa 4 usiku wa kuamkia leo ambapo chanzo cha kuporomoka kwa chumba hicho kinatajwa kwa ni mvua na maji yanayotiririshwa na mmoja kati ya majirani wa eneo hilo ambae amejenga juu ya mlima .
Wakizungumza na mtandao huu mmiliki wa nyumba hiyo Grace Mlela alisema kuwa wakati tukio hilo likitokea ndani ya chumba hicho alikuwepo mtoto wa miaka miwili ambae aliokolewa baada ya nyumba hiyo kuanguka .
hata hivyo alisema mbali ya kuwa chanzo ni mvua ila utiririshaji maji ovyo unaofanywa na mmoja kati ya wamiliki wa nyumba za jirani eneo hilo ni chanzo cha nyumba hiyo kuanguka.
Mlale amesema kuwa kutokana na tukio la kutiririsha maji ovyo wamepata kulalamika ofisi ya serikali ya mtaa ila hakuna hatua zinazochukuliwa dhidi ya mhusika.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huyo Bi. Desdelia Chahe na balozi wake Lucy Kilosa wamefika eneo hilo na kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwa kwa sasa wanajiandaa kumwita mhusika wa utiririshaji maji ovyo ili kufikishwa mbele ya sheria.