NMB TAWI LA MKWAWA IRINGA LAINGIA LAWAMANI


 nmb

Wakati serikali ikisisitiza wajasiriamali kujiunga katika vikundi ili kurahisisha kupata mikopo, Benki ya NMB Tawi la Mkwawa mkoani Iringa limedaiwa kuwa na ubaguzi kwa wafanyabiashara wakati wa utoaji wa mikopo.

Wakizungumza katika semina iliyoandaliwa na Benki ya NMB kwa wanachama wa NMB Business Club iliyofanyika katika Ukumbi wa chuo Kikuu Huria mkoani Iringa, wamesema Benki benki hiyo inaendelea kupoteza hadhi yake kutokana na kutoa mikopo kwa upendeleo na kuwatelekeza bila sababu baadhi ya wafanyabiashara wenye vigezo vyote kwa kushindwa kupata mikopo.


Wamesema mara nyingi wamekua wakipata pungufu ya kiasi cha mkopo walichokiomba bila maelezo yakujitosheleza yanayoonesha biashara zao hazijatimiza vigezo vya kupata fedha walizoomba.

Wameongeza kuwa baadhi ya wafanyabiashara wanapatiwa fedha nyingi zaidi ya shilingi milioni mia wakati katika maombi yao na miradi waliyonayo hawastahili hata kupatiwa milioni 10 hali ambayo inawafanya wafanyabiashara hao kuitilia mashaka Benki hiyo. 
 
Akijibu tuhuma hizo Dickson Pangamawe kutoka kitengo cha mikopo cha Benki ya NMB makao Makuu, amesema kuwa atahakikisha anafuatilia malalamiko ya wafanyabiashara hao ili kubaini sababu ya kupewa mkopo pungufu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo