CCM MAKETE KULA SAHANI MOJA NA VIONGOZI WAZEMBE WA SERIKALI

Katibu wa CCM wilaya ya Makete Bw. Miraji Mtaturu

Chama cha mapinduzi CCM wilayani Makete kimetoa mpango kazi wa mambo watakayoyatekeleza kwa mwaka 2013 ikiwa ni pamoja na kuisimamia serikali kutekeleza ipasavyo miradi ya maendeleo

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Katibu wa CCM wilayani Makete Bw. Miraji Mtaturu amesema mwaka 2013 ni mwaka wa kazi kwa chama hicho kuzidi kufanya kazi ikiwemo kuibana serikali pale inapozembea

Amesema kwa hivi sasa wanakwenda katika matawi yote ya chama hicho ndani ya Makete ili kuzungumza na viongozi wote wa CCM kwenye matawi kuwaagiza kuwasimamia viongozi wa serikali ili wafanye kazi kama serikali inavyotaka ili kuondoa uzembe unaoonekana kwa baadhi ya watendaji wa serikali

“Kikubwa ni kuisimamia serikali ili miradi mbalimbali itekelezwe na kwa maana hiyo tutakwenda kukutana na viongozi wote wa CCM kwenye matawi yote ili tuwaelekeze namna ya kuibana serikali kusimamia ipasavyo miradi mbalimbali” alisema Mtaturu

Ameitaja baadhi ya miradi hiyo kuwa nia pamoja na miundombinu ikiwemo barabara, ujenzi wa madarasa, zahanati pamoja na miradi ya kilimo

Katika hatua nyingine katibu huyo amezungumzia maandalizi ya maadhimisho ya miaka 36 tangu kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi ambapo maadhimisho hayo kimkoa yanatarajiwa kufanyika katika wilaya ya Makete katika kata ya Tandala

Amesema maandalizi hayo yanakwenda vizuri na maadhimisho hayo yanatarajiwa kufanyika Februari 5 na yataongozwa na kiongozi wa kitaifa wa chama hicho, ambapo kutakuwa na maandamano yatakayoanzia kwenye ofisi za CCM kata ya Tandala hadi viwanja vya chuo cha ualimu Tandala na baadaye kuwa na mkutano wa hadhara katika viwanja vya chuo hicho

Mara baada ya mkutano huo wa hadhara jioni kutakuwa na mpira wa miguu ikifuatiwa na mdahalo wa kubadilishana mawazo utakaofanyika katika ukumbi wa chuo hicho

“Niwatie shime viongozi na watu wote mfike hapo chuoni Tandala kwenye mdahalo huo wa kujadili masuala mbalimbali ili kuongeza ujuzi wa mambo yanayotuzunguka” alisema Mtaturu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo