CHRISS BROWN



NEW YORK, Marekani
USHINDI wa Tuzo ya Grammy alioupata wiki iliyopita umefanya jina la Chris Brown lipambe vyombo vya habari duniani kote, lakini wengi wakiupinga.

Hata mastaa kama Miranda Lambert na Jack Osbourne waliandika katika mtandao wa twitter kuelezea mshangao wao juu ya ushindi wa kijana huyo.

Kilichowafanya wengi wapinge ushindi huo siyo kuwa hajui kuimba, bali ni tukio alilofanya miaka miwili iliyopita la kumpiga na kumuumiza vibaya aliyekuwa mpenzi wake, Rihanna huku tuzo zikiendelea kutolewa ukumbini.

Hata hivyo, Brown amewatolea maneno makali wote wanaopinga ushindi wake, huku akijitetea kuwa kila mtu anastahili kupewa nafasi ya pili anapokosea.
Na Mwanaspoti


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo