Tani 20.6 Za Bangi Zimekamatwa mwaka 2022


Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema kuwa mapambano dhidi ya dawa za kulevya yanaendelea vyema huku akitoa takwimu zinazoonesha kuwa kwa mwaka 2022 jumla ya tani 20.6 za bangi zilikamatwa katika maeneo mbalimbali nchini.


Akizungumza katika siku ya uzinduzi wa mbio za mwenge kitaifa mjini Mtwara amesema mashamba yenye jumla ya ekari 21 ya Bangi yametekezwa kwa mwaka 2022, huku Mirungi tani 15 ikikamatwa na dawa za kulevya aina ya Heroine kilo 255 zikikamatwa pia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo