Awekewa chumvi kwenye tenki la pikipiki yake, Kisa anakemea Wizi

Kijana aliyetambulika kwa jina la George Mahundi mkazi wa kijiji cha Kiyogo kata ya Masasi Wilayani Ludewa Mkoani Njombe, amedai kuwekewa chumvi kwenye tanki pamoja na Injini ya pikipiki yake kutokana na kuwa mstari wa mbele katika kukemea matukio ya wizi kijijini hapo.


Akitoa malalamiko ya tukio hilo mbele ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya hiyo Deogratius Massawe amesema hivi karibuni walikuwa na mkutano wa kijiji ambapo waliwapigia kura watu wanaohisiwa kuwa na tabia hizo za wizi hivyo kutokana na yeye kuwa muwazi katika kuwafichua wezi hao kumepelekea kukumbwa na maswahibu hayo.

Kwa upande wake Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Ludewa Deogratius Massawe amewataka wale wote waliopigiwa kura za kuhusika na matukio ya wizi kufika katika kituo cha Polisi cha Wilaya hiyo ili kufanyiwa mahojiano huku Diwani wa kata ya Masasi Daniel Mhagama akiwaasa wananchi kufuata maelekezo waliyopewa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo