Amuua mkewe kwa jembe akimtuhumu kuchepuka


 Polisi katika eneo la Navakholo, kaunti ya Kakamega wanachunguza kisa ambapo mwanamume mwenye umri wa miaka 67, anadaiwa kumuua mkewe mwenye umri wa miaka 54.


Marehemu, Rose Atieno alikuwa amemtembelea fundi wa kushona viatu ambaye ni jirani wakati mume wake alipomvamia.

Kwa mujibu wa ripoti ya Citizen, marehemu aligongwa na jembe huku mshukiwa akimtuhumu kwa kutokuwa mwaminifu katika ndoa yao.

Kamanda wa polisi wa kaunti hiyo Joseph Kigen alithibitisha kisa hicho akisema mshukiwa atafikishwa mahakamani punde baada ya uchunguzi utakapokamilika.

Mwili wa marehemu umepelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Kakamega.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo