Waziri ang'oka na Kigogo wa halmashauri Mkoani Tabora

bushosaWaziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dk. Charles Tizeba amemsimamisha kazi Afisa ushirika wa wilaya ya Urambo mkoani Tabora Ibrahim Mbonde kutokana na tuhuma za kushindwa kusimamia maagizo ya Serikali ya uendeshaji wa vyama vya ushirika nchini ambapo pamoja na kumsimamisha kazi afisa huyo pia ameivunja bodi ya chama cha msingi cha ushirika cha Milambo kwa kosa hilo na kuwasimamisha kazi watumishi wanne wa chama hicho.
Uamuzi huo umefuatia baada ya taarifa ya chama cha msingi cha Milambo, iliyobainisha kuwa chama hicho kimemtumia mzabuni wa kusambaza pembejeo kampuni ya Petrobena East Africa ambayo haijaidhinishwa na serikali kuwa kampuni za usambazaji wa pembejeo nchini.
Kwa kuwa kilimo ndiyo uti wa mgongo wa Taifa Serikali pia imedhamilia kwa dhati kuhakikisha inatatua kero zinazowakabili wakulima.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanry naye akaahidi kusimamia ili kuhakikisha wakulima hawanyonywi hasa katika kipindi cha masoko.
Joseph Kakunda ambaye ni mbunge wa jimbo la Sikonge, ameiomba serikali ilete wanunuzi zaidi wa zao la tumbaku ili kuongeza ushindani wa bei.
Katika mkutano huo uliowakutanisha wadau wa zao la tumbaku Waziri Tizeba ameagiza kutafutwa na kwa afisa wa bank wa NMB wilaya ya Urambo anayeshughulika na mikopo pamoja na mmiliki wa kampuni ya Petrobena East Africa aliyewarubuni wakulima ili waweze kuchukuliwa hatua.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo