Bodaboda waonywa kuhusu tabia yao ya Kudeka

Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) Mkoa wa Pwani, kwa kushirikiana  na Halmashauri ya Mji Kibaha, imewapa mwezi mmoja kuanzia juzi wamiliki wa pikipiki na bajaji kukata leseni ya usafirishaji abiria.

Agizo hilo lilitolewa jana kwenye kikao kilichowakutanisha waendasha pikipiki za abiria, uongozi wa halmashauri, Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani na Sumatra.

Ofisa Leseni wa Sumatra Mkoa wa Pwani, Mwasi Christian alisema kinachofanyika ni utekelezaji wa sheria inayoeleza umuhimu wa leseni ya usafirishaji abiria.

Hata hivyo, waendesha  bodaboda  walisema muda wa mwezi mmoja waliopewa ni mfupi na kuomba kuongezewa miezi mitatu, ombi hilo lilipingwa na Sumatra.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo