TUCTA yatoa tamko

Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania TUCTA limemwomba Rais John Pombe Magufuli kulegeza msimamo wake na kukubali kukaa meza moja na viongozi wa vyama vya siasa ili kupata muafaka wa kisiasa juu ya hali inayoendelea hivi sasa nchini.

Katika tamko lililotolewa na Rais wa Shirikisho hilo Bw. Gratian Mukoba, TUCTA inaona malumbano yaliyoibuka kwa takriban wiki mbili kati ya serikali na vyama vya siasa kuelekea maandamano ya Septemba mosi mwaka huu hayana tija kwa taifa, na zaidi yanaashiria uvunjifu wa amani.

Tucta katika tamko lake imeeleza kuwa machafuko yanayoendelea katika baadhi ya nchi, chanzo chake kilionekana kama masuala madogo ambayo yangeweza kudhibitiwa, lakini yakasambaa na kuwa machafuko yasiyokwisha.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo