Polisi Wazingira nyumba Vikindu, kisa msako wa majambazi wa mauaji ya polisi Mbande

Eneo la Mtaa wa Vikindu Mashariki mkoani Pwani kwenye nyumba ya mtu mmoja aliyetajwa kwa jina la Mzee Manitu paligeuka uwanja wa mapambano baada ya polisi kuizingira nyumba hiyo na kupiga risasi nyingi hewani wakati wakimtaka jambazi anayetuhumiwa kufanya mauaji ya katika tukio la kuuawa askari polisi wanne waliokuwa wakibadilishana lindo kwenye Benki ya CRDB Tawi la Mbande wilayani Temeke jijini Dar ajisalimishe. 

Katika tukio hilo Afisa wa Polisi mwenye cheo cha ASP Thomas Njuki wa Kikosi Maalum cha Kupambana na Ujambazi inahisiwa ameuawa.

Baada ya jambazi huyo kumuua askari, jeshi la polisi liliongeza nguvu eneo hilo na kupiga mabomu na risasi nyingi hewani zilisababisha taharuki katika eneo hilo na kusababisha kila mmoja aseme lake.

Mapaparazi wetu baada ya kufika eneo hilo walitaka kuzungumzia na maofisa wa polisi waliokuwa eneo hilo akiwemo, RPC wa Pwani, Bonaventura Mushongi, Gilles na Kamishna Mwandamizi wa Jeshi hilo, Liberatus Sabas lakini wote walisema hawawezi kuongea chochote mpaka wapate ruhusa kutoka ngazi za juu kwa kuwa tukio hilo si la Kimkoa bali ni la Kitaifa.

Licha ya viongozi hao kukataa kuzungumza, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Vikindu Mashariki, Mohammed Ismaili ambaye alikuwa bega kwa bega na askari hao alisema kwenye nyumba hiyo walikuwa wakiishi wanaume 7 ambapo walikutwa wanaume 3 na wanawake 3 ambapo mwanaume mmoja aliyetajwa kumuua Afisa huyo wa Polisi alitoroka pamoja na silaha yake.

HABARI: RICHARD BUKOS/ ISSA MNALLY /GPL.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo