Jamaa akiona cha moto kwa kumpa mbwa wake jina la Rais

Mwanamume kutoka Nigeria ametiwa nguvuni baada ya kumpa  mbwa wake jina la Muhammadu Buhari

-Kabla ya kutiwa nguvuni  aliandika jina la Rais kwa pande zote za mbwa kutokana na upendo wa kazi ya Rais

Joe fortemeso Chinakwe alitiwa nguvuni baada ya kuonekana akitembea na mbwa wake aliyemwitwa Buhari.

Askari walidai kumtia nguvuni kwa kuvunja amani baada ya kutembea na mbwa huyo mahali ambapo Rais ameungwa mkono na watu wengi.

Kituo cha BBC kimeripoti Chinakwe alipendezwa sana na kazi ya Rais, jambo lililomfanya kumuita mbwa wake Buhari.
 
 Chinakwe amepokea vitisho vya kifo kutoka kwa watu asiowajua kutokana na tendo lake.
 
Mwanaume huyo mwenye miaka 30, amesema kuwa alimpa mbwa wake jina la Buhari kwasababu ya mapenzi yake kwa rais huyo 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo