Migogoro ya ardhi hasa mashamba Makete ni Ishu Kubwa, Wadau wafunguka (Audio)

Imeelezwa kuwa wilaya ya Makete mkoani Njombe inakabiliwa na mashauri mengi ya migogoro ya ardhi hasa mashamba katika maeneo mengi ya wilaya hiyo

Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa wasaidizi wa kisheria wilaya ya Makete MADIPASE Mch.Denis Sinene ofisini kwake ambapo akitoa taarifa ya mashauri waliyopokea kwenye mamalaka ya mji mdogo wa Iwawa pekee kwa ajili ya kutoa elimu kutoka kwa wananchi suala la ardhi limechukua idadi kubwa kuliko maswala Ya ndoa, mirathi, mambo ya watoto na madai mengineKutokana na kufanikiwa kuwasaidia, kuwaelimisha na kusuluhisha mashauri mbalimbali watu wengi mwenyekiti huyo amewataka wananchi kutumia huduma hiyo bure kwa kwenda katika ofisi zao ama kupiga simu ambazo wamekuwa wakizitaja katika vipindi vya mwanansheria wetu vinavyorushwa na redio Green FmMch.Sinene hakuacha kutoa wito kwa wananchi juu ya msaada huo wa kisheria wanaoutoa kwa jamiiIkumbukwe kuwa wasaidizi wa msaada wa kisheria wilaya ya Makete wapo katika kata zote za wilaya hiyo

Na Henrick Idawa


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo