Balaa Mabasi ya mabasi yaendayo haraka

Zoezi la ulipaji wa tiketi kwa mabasi yaendayo haraka,limegubikwa na dosari katika vituo mbalimbali vya DART katika jiji la Dar es Salaam ikiwemo kituo cha kimara,hatua ambayo imelazimu uongozi wa dart kuruhusu abiria kuingia ndani ya mabasi ili kusafiri bure baada ya abiria kupaza sauti zao wakilalamikia mfumo mbovu wa upatikanaji wa tiketi kwa wakati.

Licha ya zoezi la majaribio kwa mabasi yaendayo haraka kuanza wiki iliyopita siku ya Jumanne ya mei 10 mwaka huu,mtazamo wa wengi ilijua kwamba mpaka zoezi la ulipaji tiketi likianza basi hakutakuwepo kwa changamoto zozote,lakini cha kushangaza zoezi hili limegubikwa na kasoro nyingi katika maeneo mengi ya jiji la Dar es Salaam ambapo katika eneo la Kimara umati mkubwa wa abiria wamelalamikia mfumo wa upatikanaji wa tiketi huku wengine wakilalamikia kulipa nauli lakini mashine imeshindwa kusoma hivyo kutakiwa kulipa mara mbili.
 
Baadhi ya abiria  wakiwemo wazee wamedai utaratibu uliowekwa ni mbovu huku wengine wakipaza sauti zao kwamba ni urasimu,wengine wamedai kwamba wamedamka mapema kufika katika vituo hivyo ili kuwahi mapema makazini au katika shughuli mbalimbali za biashara lakini kudamka kwao mapema hakujasaidia chochote huku baadhi ya abiria katika moja ya mabasi hayo wakigoma kushuka baada ya kutakiwa kulipa nauli mara mbili huku baadhi ya abiria wakilalamikia uwepo wa wezi katika maeneo hayo baada ya umati wa watu kuongezeka.
 
Abiria walitangaziwa kuingia kwenye mabasi bure huku matangazo mengine yakifuata ili kutuliza abiria ambapo baadhi ya wadau wa usafiri pamoja na viongozi wakiwemo mkurugenzi wa DART Bwana David Mgwasa amekiri dosari kuwepo na kudai zinashughulikiwa haraka huku Mkurugenzi wa Maxmalipo nchini Mhandisi Juma Rajabu amesema wamefikia hatua za mwisho na serikali ili kupewa ruhusa ya kuanza kuuza kadi za kielektronik ambazo zitauzwa kwa abiria kwa ajili ununuzi wa tiketi ili kumaliza changamoto zilizojitokeza.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo