Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo ajiuzulu


Katibu Mkuu wa Chama cha ACT - Wazalendo, Samson Mwigamba amejiuzulu nafasi yake ili apate nafasi ya kwenda masomoni Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya.

Kwa mujibu wa ACT-Wazalendo, kamati ya uongozi imekubali maombi ya Mwigamba na kumruhusu kwenda masomoni na kuwa mchakato wa kujaza nafasi hiyo utaanza mara moja.

Naye Mwigamba ameushukuru uongozi wa chama chake kwa ushirikiano waliompatia tangu chama hicho kinaanzishwa. Amesisitiza kwamba bado ni mwanachama na ataendelea kutoa ushirikiano hata akiwa nje ya nchi.

Mwanasiasa huyo anakwenda kusoma shahada ya uzamili katika masuala ya utawala na usimamizi wa biashara (MBA) na baada ya masomo hayo ataendelea na shahada ya uzamivu (PhD).


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo