MWANAMUZIKI CHRISTINA AGUILERA APICHA PICHA AKIWA UCHI KUONESHA UJAUZITO WAKE




Mwimbaji Christina Aguilera meamua kupiga picha akiwa mtupu kwa ajili ya jarida la ‘V Magazine’ la mwezi huu.
 
Katika picha hizo, mwimbaji huyo mwenye umri wa miaka 33 na mjamzito anaekaribia kujifungua, ameonesha umbo lake akiwa na mwanae tumboni huku akiwa amejifunika sehemu ya kifua chake na mikono.
 

Inaelezwa kuwa Christina ndiye aliyemuita mpiga picha Brian Bowen Smith kwa lengo la kumpiga picha ili apate kumbukumbu pia kabla ya kujifungua.

Mwimbaji huyo ambaye ni jaji wa shindano la The Voice, tayari ni mama wa mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka sita aliyempata na mumewe wa zamani Jordan Bratman na sasa anatarajia kumpata mtoto wa pili na Matt.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo